Tuzo za BET mwaka huu zitatolewa wikend ijayo, July 28/29 mwaka huu huko
Los Angeles Marekani na kushuhudia wasanii wengi wakubwa duniani
wakiperform kwenye jukwaa hilo kubwa.

Waandaaji
wa tuzo hizo wameyataja majina ya wasanii watakaoperform ikiwa ni
pamoja na majina ya wasanii wa Afrika. Rapper toka Ghana aliyeshinda
tuzo za MTV MAMA kama msanii bora wa hip hop, Sarkodie, kundi la
Mafikizolo na msanii wa kike wa Nigeria Tiwa Savage ni miongoni mwa
wasanii watakaoperform.

Wasanii hao wanawania tuzo ya Best International Act pamoja na mkali kutoka Tanzania, Diamond.
All the Best Diamond Platinumz katika tuzo za BET kwa kuwa maoni ya
awali yanaonesha anazungumziwa zaidi kwenye mitandao kuliko wengine.
0 comments:
Chapisha Maoni