Wasanii wote wa Tanzania. Hongereni kwa kazi na namna mnavyojituma
kupitia sanaa zenu. Ni jambo zuri tena la kujivunia maana mmetambua
vipaji vilivyo ndani yenu na kuvitumia kujipatia riziki.
Kwa upande wangu, naendelea vizuri. Nawatakia heri wasanii wote Waislam
walio kwenye funga ya mwezi mtukufu wa Ramadhan. Ni mwezi ambao kwa
hakika, tunahitaji kuwa na subira na utulivu wa hali ya juu.
Nimeona ni vyema leo nizungumze na wasanii wote kwa pamoja. Ndugu zangu,
katika kila kinachofanywa na binadamu, kama akitaka kiwe na mafanikio
ni lazima kuwe na juhudi, ubunifu, nia na malengo.
Unaweza kuwa na vyote au kimojawapo ambacho kwa hakika kitakusaidia
kupata vingine kisha kupaa kwenye kilele cha mafanikio. Hapa nitoe mfano
mmoja mzuri sana kwa Diamond. Huyu bwana mdogo hana muda mrefu sana
kwenye game.
Ameibuka juzijuzi tu, lakini kutokana na juhudi, ubunifu, nia na malengo
amefanikiwa na anazidi kupaa kimafanikio. Diamond tangu ameanza na
kibao chake cha kwanza kabisa alijitahidi kuendelea kuongezeka na siyo
kupungua.
Hiyo ndiyo sababu kubwa iliyomfanya mpaka sasa anafanya vizuri
kimataifa. Kwa bahati mbaya sasa, wapo baadhi ya wasanii (hasa wa muziki
wa Bongo Fleva) wanamuonea kijicho! Nasisitiza baadhi.
Hawafurahishwi na mafanikio yake. Mbaya zaidi, sumu imesambaa sasa mpaka
kwa baadhi ya mashabiki. Chuki tu! Kwa nini yeye? Kwa nini afanikiwe
kimuziki? Kwa nini aorodheshwe kwenye kugombea tuzo? Kwa nini? Kwa
nini?!
Diamond aliposhindwa kutwaa Tuzo za MAMA zilizofanyika hivi karibuni
nchini Afrika Kusini, baadhi ya watu waliandika mambo ya ajabu sana
kwenye mitandao ya kijamii.
Wengine walifikia hatua ya kusema kuwa, eti kama Diamond angeshinda watu
wasingekunywa maji! Huo ulimbukeni tunaupata wapi ndugu zangu? Diamond
ni nani? Jibu ni rahisi tu. Ni Mtanzania.
Alhamisi, 10 Julai 2014
HOME HABARI JAMII KITAIFA SIASA BURUDANI WASANII MICHEZO ELIMU MAGAZETI MAPENZI UDAKU SKENDO KOMEDI UNAFIKI TUPA KULE...HUU NDIO UKWELI KUHUSU DIAMOND PLATINUMZ...!WASANII MNAJIFUNZA NINI TOKA KWAKE?!
17:28
No comments
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
0 comments:
Chapisha Maoni