.

Alhamisi, 10 Julai 2014

HOME HABARI JAMII KITAIFA SIASA BURUDANI WASANII MICHEZO ELIMU MAGAZETI MAPENZI UDAKU SKENDO KOMEDI UNAFIKI TUPA KULE...HUU NDIO UKWELI KUHUSU DIAMOND PLATINUMZ...!WASANII MNAJIFUNZA NINI TOKA KWAKE?!



Wasanii wote wa Tanzania. Hongereni kwa kazi na namna mnavyojituma kupitia sanaa zenu. Ni jambo zuri tena la kujivunia maana mmetambua vipaji vilivyo ndani yenu na kuvitumia kujipatia riziki.

Kwa upande wangu, naendelea vizuri. Nawatakia heri wasanii wote Waislam walio kwenye funga ya mwezi mtukufu wa Ramadhan. Ni mwezi ambao kwa hakika, tunahitaji kuwa na subira na utulivu wa hali ya juu.

Nimeona ni vyema leo nizungumze na wasanii wote kwa pamoja. Ndugu zangu, katika kila kinachofanywa na binadamu, kama akitaka kiwe na mafanikio ni lazima kuwe na juhudi, ubunifu, nia na malengo.

Unaweza kuwa na vyote au kimojawapo ambacho kwa hakika kitakusaidia kupata vingine kisha kupaa kwenye kilele cha mafanikio. Hapa nitoe mfano mmoja mzuri sana kwa Diamond. Huyu bwana mdogo hana muda mrefu sana kwenye game.

Ameibuka juzijuzi tu, lakini kutokana na juhudi, ubunifu, nia na malengo amefanikiwa na anazidi kupaa kimafanikio. Diamond tangu ameanza na kibao chake cha kwanza kabisa alijitahidi kuendelea kuongezeka na siyo kupungua.



Hiyo ndiyo sababu kubwa iliyomfanya mpaka sasa anafanya vizuri kimataifa. Kwa bahati mbaya sasa, wapo baadhi ya wasanii (hasa wa muziki wa Bongo Fleva) wanamuonea kijicho! Nasisitiza baadhi.

Hawafurahishwi na mafanikio yake. Mbaya zaidi, sumu imesambaa sasa mpaka kwa baadhi ya mashabiki. Chuki tu! Kwa nini yeye? Kwa nini afanikiwe kimuziki? Kwa nini aorodheshwe kwenye kugombea tuzo? Kwa nini? Kwa nini?!

Diamond aliposhindwa kutwaa Tuzo za MAMA zilizofanyika hivi karibuni nchini Afrika Kusini, baadhi ya watu waliandika mambo ya ajabu sana kwenye mitandao ya kijamii.

Wengine walifikia hatua ya kusema kuwa, eti kama Diamond angeshinda watu wasingekunywa maji! Huo ulimbukeni tunaupata wapi ndugu zangu? Diamond ni nani? Jibu ni rahisi tu. Ni Mtanzania.

0 comments:

Chapisha Maoni