Comment
za Facebook zaid ya 8300 na Tweet zaidi ya 8000 Marekani peke yake
zilijadili ajenda moja ya inayomhusu mtoto wa Rais Obama anaefahamika
kwa jina la Malia.
Achilia mbali "COMMENTS" za Ulimwengu mzima pamoja na "LIKES" za
mitandao mingine ya kijamii ambazo ziliacha kujadili mambo mengine na
kujadili waandishi pamoja na tukio alilofanya mtoto huyo wa kwanza wa
Rais wa Marekani.
Watoa comment hao hawakujadili kitendo
cha mtoto Malia Obama (16) kuibukia katika tamasha la muziki
lijulikanalo kama Lollapalooza ambalo lilifanyika Chicago kwa siku tatu
huku binti huyo akiwa amevalia mavazi mepesi yanayoendana na sehem
husika akiwa na marafiki zake watatu.
Pia hawakujadili
kitendo cha Ikulu ya nchi hiyo kutokutoa taarifa kuwa binti huyo
atahudhuria tamasha hilo lilioaza July 31, lililofanyika siku tatu
mfululizo.
Hata hivyo ubishani mkubwa ulitokana na
kitendo cha mitandao mingi ya habari ikiwemo Yahoo kuandika tukio la
mtoto wa Obama kumpiga teke kwa bahati mbaya binti mmoja wa Uturuki
Bridget Truskey katika harakat za kushangilia, ambapo binti huyo katika
ukurasa wake wa Twitter alieleza kufurahishwa na kitendo cha kupigwa
teke na mtoto wa Obama.
Katika comment za Facebook na
Twitter, wengi waliwalaumu waandishi wa habari kuwa wamekosa mambo ya
kuandika huku wengine wakisema waandishi wa habari hawana jipya na
taaluma hiyo inaelekea kufa.
Picha ya Selfie iliyopigwa familia ya Obama katika tamasha la Jay Z & Beyonce
Hivi karibuni familia ya Obama ilihudhuria tamasha la Jay na Beyonce
ambapo mrembo mmoja alifanikiwa kupiga picha ya SELFIE na kuiweka
instergram ambapo watumiaji wengi walishanga kwakua si kawaida, lakini
pia tamasha la Lollapalooza, mtumiaji mmoja waTwitter (Sarah)
alifanikiwa kumpiga picha Malia akiwa mdomo kwa furaha wazi katika
tamasha la Lollapalooza na kuipost.
Jumatano, 6 Agosti 2014
MTOTO WA OBAMA AMPIGA MTU TEKE
05:18
No comments
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
0 comments:
Chapisha Maoni