.

Jumamosi, 16 Agosti 2014

HATIMAYE SHILOLE ATAJA SABABU ZA KURUDIANA NA MZIWANDA!

Staa wa wimbo wa Nakomaa na Jiji, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ akiwa na mpenzi wake Nuhu Mziwanda. 
STAA wa wimbo wa Nakomaa na Jiji, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amesema sababu kubwa ya yeye kurudiana na mpenzi wake waliyegombana, Nuhu Mziwanda ni kuombwa msamaha. 

Shilole alisema mpenzi wake huyo aligundua kwamba aliteswa na wivu na kusababisha wagombane hivyo alipotambua kosa lake, aliomba msamaha wakarudiana na mambo yakawa shwari.
Zuwena Mohamed ‘Shilole’
“Kikubwa ni kwamba ameomba msamaha ndiyo maana na mimi sikuwa na hiyana, nikapatana naye siku chache tu baada ya kugombana,” alisema Shilole.Hivi karibuni wawili hao waliripotiwa kuwa wamegombana na kila mtu kuchukua hamsini zake.

0 comments:

Chapisha Maoni